AKATWA SEHEMU ZA SIRI AKIWA AMELALA KWA SHEMEJI YAKE

Mpanda Katavi

Mtu mmoja Mkazi wa Kijii cha Majimoto Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi MwamiM wanalusi (31) amekatwa nakisu katika sehemu zake za siri na watu wasiojurikana wakati akiwa amelala ndani ya nyumba ya shemeji yake na watu wasio julikan.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea hapo jana majira ya saa nane usiku nyumbani kwa shemeji yake.

Alisema siku ya tukio Mwami alikuwa ameenda kumtembelea shemeji yake aitwaye Anset Kapampala (36) ambae alikuwa akiishi katika kijiji hicho cha Majimoto.

Baada ya mlo wa usiku mwenyeji wake alimuonyesha chumba cha kulala ambacho hata hivyo hakikuwa na godoro wala kitanda bali kulikuwa na Benchi la kupumzikia ambalo shemeji yake ambae ni mwenyeji wake alimweleza Benchi hilo ndilo alitumie kama kitanda cha kulalia kutokana na hari yake ya kiuchumi kutokuwa nzuri.

Alisema wakati Mwami yuko ndani ghafla walitokea watu asio wafahamu ambao waliingia ndani ya chumba hicho na wala hawakumsemesha chochote hari ambayo ilimfanya ashikwe na butwaa.

Alieleza ndipo watu hao walipo anza kumkata kwa kisu sehemu zake za ume hadi ume ukawa umeharibika vibaya na kisha watu hao wakatokomea kusiko julikanana kumfaya yeye apige mayowe ambapo shemeji yake ambae alikuwa amelala kwenye nyumba yake nyingine alishituka na ndipo alipoingia ndani na kumkuta mgeni wake akiwa ameharibiwa vibaya sehemu zake za siri.

Kamanda Kamanda Kidavashari alisema chanzo cha tukio hilo bado hakijulikana na polisi wanaendelea na epelelezi ili kuwabaini na kuwakamata waliohusika ili sheria ichukuwe mkondo wake.

Source: Katavi Yetu blog