Afikishwa Mahakamani Kwa Kumbaka Bibi wa Miaka 90


Mkazi wa kijiji cha Bulembo makazi ya wakimbizi ya Katumba wilayani Mlele Mkoa wa Katavi Sindebula Msagi (32) amefikishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi ya wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumbaka na kumlawiti mwanamke mwenye umri wa miaka 90

Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi Ally Mbwijo aliiambia mahakama hiyo hapo juzi mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo Chiganga Tengwe kuwa mshitakiwa alitenda kosahilo hapo desemba 22 mwaka jana majira ya saa 8 usiku nyumbani kwa kikongewe huyo.

Alisema siku hiyo ya tukio mshitakiwa Sindebula alifika nyumbani kwa mama huyo na kuvunja mlango na kisha aliingia ndani ya nyumba ya mama huyo ambae alikuwa ni mgonjwa wa kupooza mguu wa kulia na mkono wa kulia kisha alimbaka na kumlawiti kwa nguvu mama huyo Pamoja na mama huyo kumsihi mshitakiwa asimfanyie kitendo hicho alimweleza kuwa umri wake ni mkubwa hasitahili kufanyiwa hivyo lakini mshitakiwa hakujali ombi la mama huyo bali aliendelea kumfanyia unyama kikongewe huyo licha ya kupiga mayowe ya kuombamsaada kwa majirani hakuweza kufanikiwa kutokana na nyumba aliyokuwa akiishi kuwa mbali na majirani


Mwendesha mashitaka aliendelea kuiambia mahakama hiyo ambayo ililazimika kwenda kusikilizia kesi kwenye eneo la tukio kutokana na hari ya mama huyo kuwa katika hari mbaya ya kiafya kuwa mshitakiwa aliendelea kumfanyia unyama mama huyo mpaka usingizi ukampata na kisha kulala ndani ya chumba cha mama huyo

Alieleza ilipofikia majira ya saa 12 asubuhi ndipo mama huyo alipoweza kufungua dirisha na aliweza kumwona mtu mmoja aitwaye Ashabola Elly aliye kuwa akipita jirani ya nyumba yake ndipo alimwonyesha ishara ya kumwita kwa kutumia vidole ili aweze kufika kumpatia msaada

Mwendesha mashtaka alisema baada ya Ashobola kuingia ndani alimkuta mshtakiwa akiwa amelala chini na ndipo alipoweza kumtambua ila hakuweza kumuamusha kutokana na tabia yake ya ukorofi hivyo ilimlazimu akimbie kwenda kutoa taarifa kwa majirani .

Majirani waliweza kufika katika eneo hilo huku wakiwa na viongozi wa kijiji hicho hata hivyo walikuta mshtakiwa amekwisha amka na kutokomea.

Alisema polisi walifanikiwa kumkamata mshtakiwa muda mfupi baada ya kuwa ametoka kwenye nyumba hiyo na katika maelezo yake ya awalai mshtakiwa alikiri kutenda kosa hilo kutokana na kile alichodai kilisababishwa na pombe nyingi ya kienyeji aliyokuwa amekunywa aina ya Kayoga


Taarifa ya daktari aliyemfanyia uchunguzi mama huyo imeonyesha kuharibiwa vibaya sehemu zake za siri na haja kubwa , katika kesi hiyo upande wa mashtaka una mashahidi wanne na mshtakiwa hana shahidi yoyote.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Chiganga aliamuru mshtakiwa kwenda Rumande hadi hapo March 28 mwaka huu kesi yake itakapaosikilizwa.



source: kataviyetu.blogspot.com