Viboko Kurudishwa Mashuleni

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imesema ina mpango wa kurudisha
viboko mashuleni kama sehemuya mpango mkakati wa kuboresha na kuinua
kiwango cha elimu nchini.
Pia imepiga marufuku matumizi ya simu za mkononi kwa wanafunzi hao
kutokana na kuchangia kuporomoka kwa elimu na maadili hali inayotishia
uwepo wa taifa la mambumbu kwa miaka ijayo.
Ni katika uzinduzi wa mfumo mpya wa usomaji kwa njia ya teknolojia ya
Habari na Mawasiliano TEHAMA baina ya Walimu na Wanafunzi wa kupitia
mtandao.
Naibu Waziri na Mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo anabainisha mipango
mipya ya kurejesha nidhamu katika masomo…
Naibu Waziri Mulugo anasema mfumo huo wa elimu kwa mtandao utasaidia
kukabili uhaba wa vitabu na kubainisha kuwa ipo haja kwa wadau wengine
kujitokeza kusaidia sekta ya elimu badala ya kuelekezalawama kwa
serikali…
Faraja Nyalandu ni Mwanzilishi wa mfumo huo na hapa anaelezea jinsi
wanafunzi watakavyonufaik ­a na mfumo huo…
Mfumo huo ni sehemu ya mpango mkakati wa kuboresha elimu bora nchini
ikiwa ni pamoja na kwenda sambamba na ukuaji wa sayansi na teknolojia
mfumo ambao umeshika kasi kwenye sekta za maendeleo ya nchi nyingi
duniani.