Jamaa Auwa Watoto Kikatili

JESHI la Polisi mkoani Katavi, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Majimoto wilayani Mlele, Justine Albert (24), kwa kosa la kuwaua kikatili watoto wake wawili kwa kuwanyonga. na kisha kumjeruhi vibaya mke na kuwatumbukiza wote katika kisima kilicho karibu na kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema mauaji hayo yalitokea saa 11:30 alfajiri usiku wa kuamkia juzi.

Inasemekana kwa muda mrefu mtuhumiwa, alikuwa akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na jirani yao na kwamba baadhi ya watoto wanadaiwa kuzaliwa nje ya ndoa yao.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya familia, watoto walionyongwa na baba yao ni Frank Justine (6),  na Elizabeth Justine (4), na mke wa mtuhumiwa, Jackline Lwiche (21) ambaye alifariki hospitali kwa matibabu.

Akisimulia tukio hilo ndugu wa Jackline anasema mama huyo ambaye alitumbukizwa kisimani akiwa hai alifanikiwa kumuokoa mtoto wake mmoja wa mwisho, Maria Justine mwenye umri wa miezi sita kwa kumtupa nje ya kisima, Maria Justine mwenye umri wa miezi sita.

Mama huyo aliyeopolewa majini na majirani akiwa hajitambui kwa kunywa maji mengi, na mtoto aliokotwa na majirani siku moja baada ya tukio akiwa na majeraha madogo mwilini mwake

Akisimulia mkasa huo, alisema kulipopambazuka baadhi ya wakazi wa kijiji hicho waliokuwa wakielekea kwenye shughuli zao, walimwona mtoto akiwa ametelekezwa kando ya njia na kumtambua kuwa ni Maria mwenye umri wa miezi sita, ambaye ni kitindamimba wa mtuhumiwa.
Inadaiwa ndipo walipoamua kufika nyumbani kwa mtuhumiwa na kumpatia taarifa hiyo na kuhoji alipo mama yake bila kupata majibu ya msingi.

Lakini mtuhumiwa aliwaeleza kuwa alikuwa ametoroka kusikofahamika na watoto wote.

Kutokana na maelezo hayo, wananchi hao walimtilia mashaka mtuhumiwa na kuamua kutoa taarifa kituo cha Polisi.

Baada ya polisi kwenda eneo la tukio, walimkuta kichanga (Maria) na kubaini ulikuwa na miburuzo ardhini na michubuko kitendo kilichowafanya wafuatilie mpaka kisimani.

Walipofika kisimani, waliamua kufungua mfuniko wa kisima hicho ndipo walikuta miili mitatu ikielea kwenye maji.

Kutokana na hali hiyo, polisi kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kuopoa miili yote, huku mama ambaye alikuwa amekunywa maji mengi akiwa taabani na kupoteza fahamu.

Kamanda Kidavashari, alisema baada ya kumuopoa mama huyo alikimbizwa kituo cha afya cha kijijini Mamba, alilazwa hapo kwa matibabu hadi mauti yalipomfika jana  jioni.



source:Katavi2date