KumbuKumbu Ya Marehemu Edward Moringe Sokoine

LEO NI KUMBUKUMBU YA MAREHEMU EDWARD MORINGE SOKOINE ALIYEFARIKI KWA
AJALI YA GARI 12/04/1984 LEO ANATIMIZA MIAKA 29

Ufuatao ni miongoni mwa maneno aliyowahi kuyatoa wakati wa Uhai wake.

"Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka
thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize
mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asimuulize mwanae, 'mali
hii umeipata wapi?'" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1983"Aliwahi
kuwa Waziri Mkuumara mbili, tangu tarehe13 Februari 1977 hadi 7
Novemba 1980, tena tangu tarehe 24 Februari 1983 hadi kifochake,
alipofariki kufuatana na ajaliya gari.
Uongozi wake ulionekana kuwa wa mfano kwa jinsi alivyokuwa na
uadilifuna kufuatilia utendaji kazi huku akikemea ulajirushwa na
ubadhirifu wa mali za umma.
Sokoine alifariki kwa ajali ya gari wakati akitoka kwenye kikao cha
bunge Dodoma kuelekea Dar es Salaam. Wengi wanashuku ajali hiyo kuwa
ilipangwa.
Kifo chake kilileta majonzi makubwa kwa Watanzania wa kawaida ambao
walikuwa wanamtarajia kuwatetea wanyonge na kuinua hali ya maisha yao.
Mwiliwa Edward Moringe Sokoine ulizikwa nyumbani kwaoMonduli, mkoaniArusha.
Chuo cha Kilimo na Mifugo Morogoro kilipewa jina la "Chuo cha Kilimo
cha Sokoine" ambacho kwa sasa ni Chuo Kikuu cha Sokoine.