Tanzania Yazidi Kufukuzia Namba za Juu

Tanzania na Timu ya taifa ya mpira wa miguu imeendelea kujichukulia
nafasi kupanda juu katika viwango vya FiFa na sasa Kukwea mpaka
kufikia Nafasi ya 116 kutoka 119 katika takwimu zilizotolewa mwezi
uliopita wa March. Tanzania Imepata Points 3 baada ya Kuichabanga Timu
ya Taifa ya Morocco kwa goli Tatu kwa moja Katika uwanja wa Taifa
Jijini Dar es salaam mwenzi March, ambapo ulikuwa na Mchezo wa
kutafuta Nafasi ya kufuzu Kucheza final za kombe la Dunia , Michuano
hiyo Itafanyika Nchini Brazili mwakani(2014). Tanzania Katika michuano
Hiyo Ipo Kundi moja na timu za taifa za Ivory coast Vinara wakiwa na
Points 7, Tanzania Yenyewe Points 6, Morocco points 2 na Gambia point
1 Huku zote zikiwa zimecheza Mechi Tatu kila mmoja.

Kwa Siku za Hivi Karibuni Taifa stars imekuwa wazuri zaidi katika
uwanja wa nyumbani kwa kuzifunga timu vigogo. Cameroon, Zambia na
Morocco