WAZIRI WA ULINZI AJIUZURU MAREKANI

Waziri wa ulinzi nchini Marekani, Chuck Hagel,amejiuzuru nafasi yake hiyo akiwa ametumia muda wa chini ya miaka miwili kazini.

Rais Barack Obama ameielezea hatua hiyo kuwa ni ya kawaida, nakumsifu Hagel kwa uamuzi aliouchukua lakini pia kwa ushauri alokuwa akimpatia na tabia yake ya ukweli na uwazi kwakipindi chote alichokuwa waziri wa ulinzi.

Lakini wachunguzi wa mambo mjini Washington wanaielezea sababu halisi ya kujiuzuru kwa waziri huyo wa ulinzi ni kushindwa kuingilia misimamo yaraisi Obama juu ya sera ya uhamiaji.

Mwandishi wa BBC mjini humo amemuelezea waziri Hagel ambaye ni M Republican kuwa alichaguliwa kuvirejesha nyumbani vikosi vya kijeshi vya nchi hiyo vilivyoko Afghanistan na nje ya hapo lakini bajeti yake ikakatwa.

Lakini changamoto hiyo inayolikabili taifa hilo kutokana na kitisho cha kikundi cha dola ya kiislam Is, mgogoro wa Syria na Urusi na uchokozi wa Ukraine inadhaniwa kuwa ni toufauti za kitaaluma na bwana Hagel ametakiwa kusalia madarakani mpaka hapo mrithi wake atakapoteuliwa na baraza la Seneti.