WATUPWA JELA KWA KUCHEZA WATUPU KWENYE VIGODORO

WAKAZI wanne wa eneo la Masasi Mbovu katika Halmashauri ya mji Masasi mkoani Mtwara wamehukumiwa kifungo cha miezi sita jela kwa kosa la kucheza wakiwa watupu kwa mtindo wa 'vigodoro' kwenye sherehe ya ndoa.

Akitoa hukumu hiyo juzi hakimu wa mahakama ya wilaya ya Masasi, Halfani Ulaya alisema watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Septemba 30 mwaka huu kwa makusudi hukuwakijua ni kosa la jinai na ukiukwajiwa maadili ya kitanzania.

Waliohukumiwa kwenda jela ni Anna Yohana (25), Aziza Chukachuka (20) Jemima Jordan (22), huku mtuhumiwa mmoja ambaye ni mtoto mwenye umri wamiaka 17 (jina limehifadhiwa) akitakiwa kulipa faini ya Sh 50,000 kutokana na umri wake kuwa mdogo.

Kwa mujibu wa hakimu Ulaya, ameridhishwa na upande wa utetezi ulioletwa na mashahidi watatu mahakamani hapo na kwamba uamuzi huo ni wa haki na kisheria kwani walitenda kosa la jinai namba 167 ya mwaka 2014.

Washtakiwa hao walipotakiwa kujitetea hawa kusema chochote na kwamba wote wamekiri kuwa kwa makusudi walitenda kosa hilo huku mahakama ikitoa onyo kali kwa watakaobainika kuendelea na vitendo hivyo vinavyokwenda kinyume na maadili ya Watanzania.