WANAJESHI WAANDAMANA IVORY COAST

Wanajeshi nchini Ivory Coast wameingia ndani ya majengo ya radio ya taifa hilo katika mji wa Bouaké kutokana na maandamano yao ya kudai maslahi zaidi ya kazi.

Hata hivyo wanajeshi hao wamerekodi ujumbe wa madai yao, unaosisitiza wafanyakazi kuondoka katika vituo vyao vya kazi.

Waziri wa Ulinzi Ivory Cost Paul Koffi amewataka waandamanaji hao waliopo katika mji wa Bouaké na Abidjan kurejea kazini mara moja.

Ripoti zinasema kuwa lingekuwa jambo la msingi kama angelitoa ahadi ya kulipa madai ya wanajeshi hao na kuboresha mazingira ya huduma za afya na mafao mengine.

Jeshi la Ivory Cost linajumuisha askari wa zamani na wengine wakiwa ni waasi waliojiunga na jeshi la serikali kuunda jeshi jipya baada ya mgogoro wa Ivory Cost kumalizika mwaka 2011 uliokuwepo kati ya Alassane Ouattara na mtangulizi wake Laurent Gbagbo.