KIKAO CHA BUNGE CHASAMBARATISHWA KWA MABOMU YA MACHOZI

Polisi katika mji mkuu wa Lagos, Nigeria, wamefyatua gesi ya kutoa machozi ndani ya jengo la bunge, na kulazimisha kuahirishwa kwa mjadala muhimu wa bunge hilo kuhusu kurefushwa kwa kipindi cha hali ya tahadhari kaskazini mwa nchi hiyo.

Mwaandishi wa BBC amesema kuwa maafisa wa Polisi walikuwa wakijaribu kumzuia spika wa Bunge la waakilishi Aminu Tambuwal, ambaye alihamia chama cha upinzani mwezi uliopita kuendelea na mjadala huo.

Wabunge wa upinzani wanasema kuwa hali ya tahadhari imeshindwa kuhimili visa vya wapiganaji wa kiislam wa Boko Haram.

Mwaandishi wa BBC aidha anaongeza kuwa afisa mkuu wa polisi ametakiwa kufika mbele yabaraza la Senate kuelezea hatua hiyo ya maofisa wa polisi kurusha vitoa machozi ndani ya Bunge.

Bunge limefungwa hadi juma lijalo.