"HATURUHUSU VITENDO VYA NGONO MAGEREZANI"

WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imeendeleza msimamo wake kuwaTanzania bado haina sheria ya kuwaruhusu wafungwa kukutana kifaragha na waume au wake zao.Hii ni mara ya tatu kwa serikali kutoa majibu hayo kutoakana na maswaliya wabunge, ambako mara kadhaa swali hilo limekuwa likiulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu Mariam Msabaha (CHADEMA).

Jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereila Ame Silima, alikiri kuwa Tanzania haina sheria hiyo na akajibu kuwa, ujauzito ambao huwapata wafungwa wanawake, unatokanana kuupata nje ya magereza.

Alitoa majibu hayo kutokana na swali la Mbunge wa Viti maalum, Rukia Kassim Ahmed (Cuf), ambaye alitaka kujua ni kwa namna gani wafungwa wanawake wanapata ujauzito wanapokuwa ndani yamagereza yao.

Mbunge huyo, pia alihoji kama magerezani kuna usiri, ni kwa namna gani mahabusi ambao ni mashehe kutoka Zanzibar wanafanyiwa vitendo vya ulawiti gerezani.

Naibu Waziri huyo, alisema kuwa Jeshi la Magereza lina utaratibu wa kutenganisha wafungwa wa kiume na wa kike, kwani kilawatu hutunzwa kwa sehemu zao na hulindwa na watu wa jinsia zao.

Kuhusu tuhuma za kulawitiwa kwa Mashehe wa Zanzibar, Waziri wa Mambo ya Ndani Mathias Chikawe, alisema kuwa sakata la Sheikh Salum Ali Salumu, linafanyiwa kazi na kwamba kiongozi huyo ameshafanyiwa uchunguzi wa awali katika hospitali ya Amana.

"Jambo hilo lipo mikononi mwetu, tumempeleka hospitali ya Amana nakesho (leo) tutampeleka hospitali ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi, lakinitunachunguza pia tabia ya kiongozi huyo na mwenendo wake kabla ya kuingiagerezani," alisema Chikawe.

Hata hivyo, Chikawe alisema kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kwa watuhumiwa hao, kwani tangu mwanzo hakuwa ameripoti vitendo hivyo lakini alipofika mara ya nnegerezani ndipo akaripoti kufanyiwa vitendo hivyo na mmoja wa askari polisi.