'OPERATION LIKOFI' VIJANA WALIKUFA KIHOLELA

Ripoti ya shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu Human Rights Watch inasema polisi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kwa jumla wamewaua vijana wapatao 51 katika operesheni ya kupambana na uhalifu Kinshasa.

Watu wengine 33 hawajulikani waliko tangu operesheni hiyo ilopewa jina "Operation Likofi", ilioidhinishwa Kinshasa mwaka uliopita kufanyika.

Human Rights Watch liliwahoji zaidi ya maafisa 100 wa polisi, watu walioshuhudia nauaji hayo pamoja na jamaa wa waathiriwa.

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, liliwahoji zaidi ya maafisa 100 wa polisi , walioshuhudia matukio pamoja na jamaa wa waathiriwa waliotoa taarifa ya kile kilichosemekana kuwa mauaji ya kiholela.

Msemaji wa shirika la hilo,(Anneke Van Woudenberg), alituhumu serikali kwa kuficha taarifa kuhusu mauaji hayo na kusema familia za waathiriwa zilikuwa zimetishwa na kuonywa dhidi ya kufichua taarifa za mauaji hayo.

Ripoti iliyotolewa na umoja wa Mataifa mwaka jana pia ilielezea kuhusu mauaji hayo.