MAHAKAMA YACHOMWA MOTO TARIME

MAHAKAMA ya Mwanzo ya Riagoro wilayani Rorya mkoani Mara, imechomwa moto na watu wasiojulikana na mali na nyaraka mbalimbali zilizokuwao, zimeteketea.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Lazaro Mambosasa alisema tukio hilo ni lausiku wa kuamkia Novemba 8.

Uchunguzi wa awali unaonesha mahakama hiyo, haina umeme na inasadikiwa huenda imechomwa nawahalifu wanaotuhumiwa katika mahakama hiyo.

Moto huo uliteketeza samani na vielelezo katika ofisi ya makarani. Hata hivyo, kwa upande wa ofisi yahakimu, mafaili yalinusurika kuteketea baada ya wananchi kufika na kuzima moto huo wakisaidiana na polisi wa Kituo cha Utegi.

"Tumepeleka askari wetu wa uchunguzi katika maeneo hayo ili kuweza kupata wahusika ili waweze kufikishwa katika vyombo vya sheria," alisema Mambosasa.