KAULI NA MSIMAMO YA MWIGULU NCHEMBA NDANI YA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI YA CCM KUHUSU WIZI WA ESCRO

KAULI NA MSIMAMO YA MWIGULU NCHEMBA NDANI YA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI YA CCM KUHUSU WIZI WA ESCROW

"CAG ameshasema pesa zile zilikuwa mali ya umma, sasa zikamatwe zote na wahusika wote wakamatwe,"

"Nimemwagiza Kamishna wa Kodi amfukuze kazi yule mtumishi wa TRA iliyoko chini ya wizara yangu anayetajwa kuchota Bilion 1.6 na afilisiwe, pia mitambo na kodi vikamatwe na wahusika wakamatwe.

"Hatuwezi kuendeleza mazoea ya kufunga maskini na kuwapa likizo wezi wakatumie fedha. Walio serikalini na walioko kwenye siasa wakamatwe na tuwafilisi fedha irudi serikalini,"

"Tazama wanafunzi, watoto wa maskini zaidi ya elfu 40 wamekosa mikopo, madawa hospitalini hakuna, maskini wanakufa, watu wasio na hatia wanafungwa kwa kukosa michango ya maabara, walimu wanadai fedha zao, wazabuni wanauziwa nyumba zao na benki huku wakiidai Serikali kwa huduma walizotoa, leo wezi tuwape adhabu ya kujiuzulu? Tuwape likizo ya kwenda kutumia fedha walizo waibia maskini?"