MBOGO AJERUHI WANNE

Watu wanne kutoka kijiji cha Namabengo Wilaya ya Namtumbo Wamejeruhiwa na Nyati na kusababishiwa kulazwa katika kituo cha Afya Namabengo Mkoani Ruvuma.

Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msekhela amesema watu walio jeruhiwa walikuwa katika shuguli za kawaida za kila wakipalilia makaburi,wengine kuloweka mihogo bila kujua ndipo walipovyamiwa na Nyati.

Kamanda wa Police Mihayo Msekhela amesema Jeshi la Police lilipo pata Tarifa Hiyo lilichukua Hatua Mara Moja na kushirikiana na Askari wa wanyama Pori kumsaka Nyati huyo hatimaye kuweza kumuua.