MABEHEWA 50 KATI 274 YA MIZIGO YAWASILI

Mabehewa Hamsini kati ya 274 ya kusafirishia mizigo katika Reli ya Kati yamewasili nchini kutoka India na mabehewa 22 ya abiria yana tarajiwa kuwasili Desemba mwaka huu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dakta SHABANI MWINJAKA amesema kuwasili kwa mabehewa hayo kutaokoa kwa kiasi kikubwa miundombinu ya barabara ambayo huharibika muda mfupi baada ya kutengenezwa kutokana na malori ya mizigo kwani kwa sasa mizigo yote itasafirishwa kwa njia ya reli.

Amesema Kampuni ya Reli Tanzania imetengewa zaidi ya shilingi bilioni 45 kwa ajili ya kuboresha huduma zake ikiwa ni pamoja na kununua vichwa na mabehewa mapya.

Amesema hadi mwaka 2015 injini 45 zitakuwa z imekamilika amba zo z itawezesha kusafirisha tani milioni 1.5 na kuongeza kuwa u jenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es salaam kwenda Kigoma, Tabora hadi Mwanza na Uvinza Msongati hadi B urundi utafanyika.

Mkurugenzi M tendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania Mhandisi KIPALLO KISAMFU amesema injini nne zilizokuwa zikitengenezwa mkoani Morogoro zimekamilika na nyingine 15 zinatengenezwa Afrika ya Kusini ambazo zitagharimu shilingi bilioni 70.