KOREA KASKAZINI KUPELEKWA ICC?

Baraza la umoja wa mataifa la haki za binadamu limesema Korea Kaskazini inastahili kufikishwa katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu kutokana na kukiuka haki za binadamu.

Katika baraza hilo zimetolewa tuhuma dhidi ya Korea Kaskazini kwamba serikali yake imekuwa ikifanya vitendo vya ukiukaji haki za binadamu.

Mapendekezo hayo yaliyopitishwa na baraza la haki za binadamu la kimataifa yanapaswa kupigiwa kura ili kupitishwa na bunge yaweze kuhalalishwa.

Ripoti ya mwezi Februari mwaka huu iliyotolewa na umoja wa mataifa ilibainisha kuwa watu wa Kawaida Korea Kaskazini wanakabiliwa na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu napia mauaji.

Umoja wa mataifa unafanya uchunguzi dhidi ya Korea Kaskazini ili kupata ushahidi wa majina ambayo yapo kwamba taifa hilo limeua, likitesa watu,ukatili wa kisiasa na uhalifu mwingine.

Hata hivyo China na Urusi wanaoshikilia kura ya Veto katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wamepingana na mapendekezo hayo ya Baraza la Usalama, huku nayo Korea Kaskazini ikiipinga ripoti hiyo.

Wanadiplomasia wana wasiwasi kuwa huenda China inataka kutumia kura yake ya Veto kupinga Baraza la Usalama kupeleka kesi zake katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC.