MBUNGE KEISSY ANUSUSIKA KICHAPO TENA

Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy almanusura azue kizaazaa kwa mara nyingine na wabunge wa Zanzibar alipohoji sababu ya wabunge hao kuzungumzia suala la Rais Jakaya Kikwete kwenda kutibiwa Marekani akisema wenyewe wamekuwa wakienda kutibiwa India.

Mbunge huyo amekuwa akiingiakatika mgogoro na wabunge wa Zanzibar kuhusu masuala mbalimbali. Kwanza ilikuwa katika Bunge la Bajeti lililopita, alipochangia Bajeti ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akihoji mchango wa Zanzibar katika wizara hiyo na mwisho ilikuwa katika Bunge la Katiba alipokuwa akichangia suala la Muungano.

Jana, Kessy alisema hayo wakatiNaibu Spika, Job Ndugai alipokuwa akijibu miongozo mbalimbali ya wabunge walioiomba baada ya kipindi cha maswali na majibu kitendo ambacho kiliwafanya wabunge karibu wote wa upinzani kusimama wengine wakitaka atolewe nje.

Wakati Ndugai akiendelea kusikiliza miongozo hiyo, Kessy alisimama na kupewa nafasi kisha kusema: "Hao wanapiga kelele kwa nini Rais amekwenda kutibiwa Marekani mbona wao wamekwenda kutibiwa India? Tena nawafahamu wabunge kama sita hasa wa CUF, sasa Rais kaenda kutibiwa Marekani mnahoji, je, mlitaka akatibiwe Zanzibar? Kauli hiyo iliamsha hasira za wabunge wa upande wa upinzani ambao walisimama wakitaka Keissy achukuliwe hatua za kinidhamu.

Rais Kikwete yuko Marekani baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume kwenye Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko Baltimore, Maryland ambako taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana,ilisema hali yake inaendelea kuimarika na alianza kufanya mazoezi ya kutembea tangu juzi.

Baada ya wabunge wa upinzani kusimama akiwamo David Kafulila (Kigoma Kusini - NCCR Mageuzi), David Silinde (Mbozi Magharibi - Chadema) na wengine wakitaka Kessy atimuliwe, Ndugai aliwaomba kuwa watulivu huku Kessy akiamua kutoka kwenye Ukumbi wa Bunge.

Wakati Kessy akitoka, Mbunge wa Konde (CUF), Khatib Said Haji alinyanyuka na kuonekana kumfuata lakini alizuiwa na walinzi pamoja na Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), Ismail AdenRage na kumrudisha huku Keissy akisindikizwa na Mbunge wa Sikonge (CCM), Said Nkumbana mmoja wa walinzi wa Bunge.


Miongozo mingine

Katika miongozo ya awali, baadhi ya wabunge walitaka Serikali kutoa tamko kuhusu ununuzi wa mahindi ya wananchi hasa baada ya kuzalishwa mengi na kukosekana kwa soko, pia wengine wakitaka tamko la Serikali kuhusu tatizo la dawa tiba nchini kiasi cha kufanya wananchi kukosa matibabu.

Silinde alitaka kauli ya Serikali kuhusu ununuzi wa mahindi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Marc Mwandosya alisema wizara husika itatoa tamko hilo wiki hii... "Napenda niwaambie waheshimiwa wabunge kuwa Serikali imesikia na itatoa tamko la suala la mahindi wiki hii."

Wabunge wa Viti Maalumu, Ester Bulaya (CCM) na Rukia Kassim (CUF) walitaka tamko la Serikali kuhusu tatizo la dawa nchini na hasa deni la Bohari yaKuu ya Dawa (MSD) pamoja na kukosekana kwa mashine ya mionzi katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road.

Akijibu swali hilo, Profesa Mwandosya alisema Serikali piaitatoa tamko kuhusu hali ya tibaya saratani nchini, madaktari namipango iliyopo katika kupambana na tatizo la kukosekana kwa mashine ya mionzi Ocean Road... "Tutatoa tamko kuhusu hayo katika bunge hili."

Akizungumzia mwongozo huo, Ndugai alisema: "Kwa vile Serikali itatoa tamko, tuiombe ilete mapema suala hilo kwa kuwa limekuwa likitusumbua hapa bungeni."