WATU WAWILI WAUAWA, MMOJA ACHINJWA

Watu wawili wamefariki dunia mkoani Iringa katika matukio mawili tofauti, likiwamo la Maurisia Malangalila aliyeuawa kwa kuchinjwa shingo kama kuku na kitu chenye ncha kali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba Maurisia (65), mkazi wa kijiji cha Bumulianga, Tarafa ya Malangali, inadaiwa aliuawa na Patrick Ngelenge.

Alisema mauaji hayo yalitokea Novemba mosi, saa tatu usiku kijijini hapo wakati marehemu alipokuwa nyumbani kwake.