KESI YA SITTI MTEMVU YANUKIA

Kesi ya sakata la kudanganya umri ambalo linamkabili aliyekuwa miss Tanzania mwaka 2014 Sitti Mtemvu linakaribia kufunguliwa baada ya uchunguzi unaofanywa na RITA kuelekea ukingoni.

Habari toka RITA zimeeleza kuwa taasisi hiyo iko katika hatua za mwisho za kukamilisha taarifa za uchunguzi kwa kuangalia wote waliohusika kudanganya umri na kumpatia Sitti cheti kipya kilichotolewa septemba 9, mwaka huu ambacho kinaonesha amezaliwa mei 31,1991.