WAFUGAJI WAVAMIA SHAMBA LA MUWEKEZAJI NA KUCHOMA MOTO

Wafugaji wa jamii ya kimasai kutoka wilaya ya Longido Mkoani Arusha wamevamia shamba la mwekezaji la Ndarakwai katika wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro na kuchoma moto baadhi ya maeneo na kuharibu mali mbalimbali kwa madai ya kugombania mipaka kwa ajili ya maeneo ya malisho.

Baadhi ya wananchi wamesema kundi la Wamasai kutoka vijiji vinavyozunguka shamba hilo ambalo liko Jirani na wilaya ya longido lilivamia eneo hilo wakiwa na mifugo yao na kuanza kuchoma baadhi ya mali za mwekezaji huyo, magari na nyumba za watalii kwa madai kuwa mwekezaji huyo ameoongeza maeneo ya mipaka.

Wamesema ni vema serikali ikachukua hatua ya kukutana na wananchi hao na kuwasikiliza ili kutatua mgogoro huo ambao umeaanza kuhatarisha amani.

Kutokana na mgogoro huo Mkuu waMkoa wa Kilimanjaro Bw.Leonidas Gama akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kilimanjaro amelazimika kutembelea maeneo hayo na kusema kuwa kitendo kilichofanyanywa na wafugaji hao hakikubaliki na kwamba wote waliohusika lazima wachukuliwe hatua za kisheria kutokana na shamba hilo kuwa na makundi ya wanyamapori 65 wakiwemo Tembo,Twiga na Pofu.