HABARI NJEMA KWA WASTAAFU

SERIKALI imeongeza kima cha chini cha malipo ya pensheni kwa wastaafu kuanzia mwaka wa fedha ujao.

Kwa sasa wastaafu wanalipwa pensheni ya sh 50,000 kwa mwezi, ambazo hulipwa kila baada ya miezi mitatu, lakini kuanzia mwaka wa fedha wa 2015/16 watalipwa katika kiwango kipya cha juu.

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, alisema hayo juzi wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge waliochangia mjadala kuhusu mapendekezo ya serikali ya Mpangowa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka 2015/2016.

Waziri Saada, alisema kiwango hicho kipya cha pensheni kitakachoongezwa kwa wastaafu hao kitatangazwa katika kipindi cha bajeti ya mwaka 2015/2016, mwakani.

"Mheshimiwa Spika, uamuzi huo umefikiwa baada ya kuona kiwango cha pensheni cha sasa chash 50,000, hakistahili kuendelea kulipwa kwa wastaafu kwa sababu hakiendani nahali ya maisha," alisema.

Pia, alisema deni sahihi, ambalo Bohariya Dawa (MSD), inaidai serikali ni sh bilioni 81 na kwamba,kati ya fedha hizo, sh bilioni 37 zimehakikiwa na kuanzia juzi sh bilioni 20 zimelipwa.

Waziri Saada, alisema mwezi ujao wataendelea kulipa sehemu nyingine ya deni hilo ambalo limetokana na uzembe uliofanywa na baadhi ya watendaji kutofuata taratibu.

Alisema kuanzia sasa,wizara yake itahakikisha taratibu zinafuatwa ili tatizo lililojitokeza lisijirudie.