TETESI SHERIA MPYA DHIDI YA USHOGA UG

Suala la wapenzi wa jinsia moja na sheria nchini Uganda baado linazua mijadala nchini humo.

Miezi mitatu tangu mahakama nchini humo kuibatilisha sheria dhidi ya ushoga kwa sababu za kiufundi sasa habari zingine zimeanza kujitokeza kuhusu uwezekano wa serikali kuleta tena muswada huo bungeni.

Kujitokeza tena kwa suala hilo wakati huu ni baada ya hati maluum kuvujishwa. Hati hiyo yakurasa tano ni ya muswada jaribio kuhusu suala la mapenzi ya watu wa jinsia moja.

Hati hiyo inaitwa : 'Mswada wa mwaka 2014 kuzuia kueneza visa vya kujamiiana ambavyo si asili wa mwaka wa 2014.

Katika hati hiyo kuna pendekezo la kifungo cha miaka saba ikiwa mtu atapatikana na hatia ya kile kinachoweza kuitwa kufagilia ushoga.

Neno lilotumiwa ni kutangaza na hivyo kutiliwa mkazo badala ya sheria ya zamani iliokuwa inatilia mkazo ushoga wenyewe.

Wachambuzi wanasema kuwa hati hii ikipasishwa kama sheria itakuwa mbaya zaidi ya ile iliobatilishwa kwani itawahukumu watu wengi mkiwemo vyombo vya habari pamoja na watu wote wanaotumia mitandao yote ya kijamii.

*'Sheria mbadala kali zaidi?'

Hati hii inasema kuwa mtu yeyote akipatikana na hatia atahukumiwa kifungo cha miaka saba.

Sheria iliobatilishwa na mahama mapema Agosti mwaka huu miongoni mwa mengine ilikuwa inasema yeyote akipatikana na hatia atafungwa jela maisha.

Waziri wa taifa wa sheria na naibu mwanasheria mkuu Fred Ruhindi akizungumza na BBC kwasimu amekataa kutoa kauli kwa kile alichoita hati iliovujishwa na kusema kuwa mchakato kuhusu sheria mpya ya kudhidbiti ushoga unaendelea.

Yeye waziri anaehusika na maadili Padri Lokodo amesema hajui lolote kuhusu hati hiyo.

*Hatua zilizofuata

Punde baada mahakama kubatilisha sheria hiyo mapema mwezi Agosti mwaka huu, chama tawala cha NRM kiliunda kamati maalum ya watu 10, ikiongozwa na makamu wa rais Edward Sekandi, kutahmini muswada hatua hiyo.

Hadi sasa haijatoa taarifa yoyote kuhusu kazi yao mpaka muda huuambapo hati ya mwaswada kuvujishwa.

Mchakato wa kuunda sheria dhidiya ushoga ilianza mwaka wa 2009 na imepitia awamu kadhaa kutokana na utata wa suala hilo.

Huku wanaounga mkono kuweka sheria kali dhidi ya mapenzi hayo, baadhi ya makundi ya kutetea haki za binadamu pamojana mataifa ya magharibi yanapinga hilo yakisem ani kugandamiza haki za bindamu.

Na serikali pamoja na mashirika ya misaada ya kimaghari yamekata miaaada kwa serikali ya Kampala kuhusiana na suala la mapenzi ya watu wa jinsia moja.Na hivyo suala la mapenzi hayo baado linavuma Uganda.