Tanzania Yasaini Mkataba wa Kudhibiti Biashara ya Silaha

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
imekuwa miongozi mwa nchi za
kwanza kutia sahihi Mkataba wa
Kimataifa wa Kudhibiti Biashara ya
Silaha Duniani ( ATT)
Utiaji sahihi wa tukio hilo la kihistoria
umeziduliwa jana jumatatu ( Juni 3)
hapa Makao Makuu ya Umoja wa
Mataifa. Ukishuhudiwa na viongozi
mbalimbali akiwamo Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon.

Katika tukio hilo Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania iliwakilishwa na Balozi
Ramadhan M. Mwinyi, Naibu
Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania
katika Umoja wa Mataifa.

Utiaji sahihi wa mkataba huo
unafanyika ikiwa ni takribani miezi
miwili kupita tangu Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa lilipoupitisha kwa
kuupigia kura 154 za ndiyo na hivyo
kuhitimisha majadiliano ya uundwaji
wa mkataba yaliyodumu kwa takribani
miaka sita.

Kutiwa sahihi kwa Mkataba huo sasa
kunafungua fursa ya kuanza kufanya
kazi rasmi baada ya siku 90, kwa
sababu zilikuwa zikihitajika sahihi 50 ili
upate baraka ya kuanza rasmi. Lakini
idadi hiyo imepitiliza katika siku ya
kwanza ya utiaji wa sahihi na kufikia
nchi 67.

Dhumuni kuu la mkataba pamoja na
mambo mengine ni kusimamia na
kuratibu biashara ya silaha za aina
mbalimbali zikiwamo, mizinga ya kivita,
magari ya deraya, ndege za kivita,
helkopta za mashambulizi, meli za
kivita, makombora pamoja na silaha
ndogo ndogo na nyepesi.

Aidha Mkataba pamoja masuala
mengineyo hautaingilia uhuru wa nchi
kununua silaha kwa matumizi yake ya
ndani na haki ya kujilinda na kulinda
mipaka yake, vilevile mkataba hauzui
nchi kufanya biashara ya kusafiri aina
yoyote ya silaha ilimradi inazingatia
sheria na taratibu zilizomo ndani ya
mkataba ikiwa ni pamoja na taratibu
ambazo nchi yenyewe imejiwekea.

Matumaini ya Jumuiya ya Kimataifa ni
kwamba utekelezaji wa mkataba na
kama utaekelezea ipasavyo utasaidia
sana kudhibiti silaha zisiangukie
mikononi mwa makundi mbalimbali ya
kihalifu yakiwamo ya kigaidi.

Akizungumza mara baada ya kutia
sahihi, Balozi Ramadhan Mwinyi
aliungana na wasemaji wengine katika
kukaribisha hatua hiyo muhimu. Huku
akieleza kwamba kwa Tanzania kutia
sahihi ni uthibitisho wa utayari wake
wa kuutekeleza kwa kuzingatia
masharti na matakwa yanayoendeana
na mkataba huo.

Akasema Tanzania imekuwa miongoni
mwa nchi za mwanzo kutia sahihi
mkataba huo kwa kuwa ilikuwa moja
kati ya nchi zilizodhamini Azimio la
Kuanzishwa kwa Mkataba na pia
ilishiriki kikamilifu katika majadiliano
yote yaliyozaa mkataba huo.

Balozi Mwinyi akaeleza pia kuwa
kufanya kazi kwa Mkataba huo
kutachangia katika amani ya Kimataifa,
amani na usalama wa Kikanda na pia
utachangia sana katika kupunguza
madhara yatokanayo na biashara
haramu na holela ya silaha lakini pia
utasaidia katika kukuza na kuimarisha
uhusiano mzuri miongoni mwa nchi
wanachama.

Katika hatua nyingine Muwakilishi huyo
wa Tanzania amesisitiza haja na
umuhimu wa uwepo wa fursa sawa
kati ya wasafirishaji wa silaha na
waagizaji wa silaha na kwamba
Mkataba huo usidhibiti au kuzuia
biashara ya silaha ambayo ni halali na
kwamba mkataba haupashwi kuingilia
au kwa namna yoyote ile au kuadhiri
uhuru na haki ya nchi kujilinda na
kulinda watu wake.

Tanzania pia imekaribisha misaada ya
kiufundi katika maandalizi ya utekelezaji
wa mkataba huo hasa kwa nchi
zinazoendelea.

Nchi hizo 67 ambazo zimetia sahihi ni ,
Albania, Antigua and Barbuda,
Argentina, Australia, Austria, Bahamas,
Belgium, Belize, Benin, Brazil, Burkina
Faso, Burundi, Chile, Costa Rica, Cote
D' Ivoire, Croatia, Cyprus, Czech
Republic , Denmark, Djibout, na
Dominica Republic.
Nyingine ni Estonia, Finland, France,
Germany, Greece, Grenada, Guyana,
Hungary, Iceland, Italy, Jamaica, Japan,
Latvia, Liechtenstein, Lithuania,
Luxembourg, Mali, Malta, Mauritania,
Mexico na Montenegro.
Mataifa mengine ni Mozambique,
Netherlands, New Zealand, Norway,
Palau, Panama, Portugal, Republic of
Korea, Romania, Saint Lucia, Saint
Vincent and the Grenadines, Senegal,
Seychelles, Slovenia, Spain, Suriname,
Sweden, Switzerland, Togo, Trinidad
and Tobago, Tuvalu, United Kingdom
of Great Britain and Northern Ireland,
United Republic of Tanzania na
Uruguay.