Majambazi Wauwa na Kupora

Watu watano wanaosadikiwa
kuwa majambazi wakiwa na silaha
mbili bunduki  aina ya SMG
wamemuwa kwa kumpiga risasi
mbili tumboni Juma  Mabula ( 36)
mfanyabiashara wa Bariadi
Shinyanga na kumpola mamilioni
ya fedha ambazo kiasi chake
hakija fahamika  na kumjeruhi
kwa kumpiga  risasi mbili
tumboni Cosmas Michael ( 28)
mfanya biashara wa Bariadi
Shinyanga  na kumpora fedha
tasilimu milioni tatu.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa
Katavi Dhahiri Kidavashari
alisema tukio hili lilitokea  juzi
majira ya saa mbili usiku  katika
kijiji  cha Itunya  kata  ya
Kapalamsenga Tarafa ya Karema
wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi
Alisema majambazi hao  kabla ya
kufanya tukio hilo waliwavamia
Adolfu John (20 ) na kumpora
fedha  tasilimu Tsh 4, 000, 000/=
na Richard Charles (25)
alimporwa  Tsh 5,000,000/= ambao
ni wafanya biashara na wakazi
wa Kijiji cha Kakese Wilaya  ya
Mpanda
Kidavashari alieleza kuwa
wafanya biashara hao walikuwa
wamekwenda kijijini hapo kwa
lengo la kununua zao la mpunga
linalopatikana kwa wingi kwenye
kijiji hicho  na ndipo walipo patwa
na tukio hili.

Alisema katika eneo la tukio hilo
liliokotwa ganda moja la risasi
aina ya bunduki ya SMG
lililotumika likiwa karibu  na
mwili wa marehemu Juma Mabula
Baada ya jeshi la polisi kupata
taarifa lilifika katika eneo hilo la
tukio na waliendesha msako
mkali  na kuwakamata watu
wanne kuhusiana na tuhuma  za
tukio hilo
Kamanda Kidavashari aliwataja
watu hao wanao shikiliwa na
polisi kuwa ni Mussa Mathias
(36), Ngusa Tola (37),  na Shinde
Jiyaago ( 34) wote wakazi wa
kijiji cha Nkuswe Tarafa ya
Karema wilayani hapa na Doto
Kayungilo (25) Mkazi wa kijiji
cha Mnyamasi Tarafa ya Kabungu.

Alisema majeruhi Cosmas
Michael ambaye amelazwa katika
Hospital ya Wilaya ya Mpanda
anaendelea kupata matibabu na
hali yake inaendelea vizuri
Kamanda Kidavashari amewataka
wananchi wa Mkoa wa Katavi
kuwabaini wageni wanaofika
kwenye maeneo yao na kutoa
taarifa kwa Jeshi la Polisi  za
kuwaarifu watakao wabaini au
kuwatilia shaka watuhumiwa ili
waweze kukamatwa  kabla ya
kutenda tukio.