Majasusi Wajipanga Kiusalama Ziara ya Obama

Idara ya Ujasusi ya Marekani
imeweka bayana kwamba inajitegemea kwa
ulinzi katika ziara nzima ya Rais Barack Obama
kwa nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, Afrika
Kusini na Senegal.

Kwa mujibu wa taarifa ya idara hiyo, katika
kuhakikisha usalama wa kutosha wakati wa
ziara ya Obama tayari maofisa wao
wameshakamilisha maandalizi ya kiusalama
katika nchi zote anazotarajiwa kutembelea.

Meli ya kivita kutua bandarini
Katika kuchukua hatua hizo, meli kubwa kabisa
ya kivita yenye hospitali maalum zipo tayari kwa
ya kambi maalumu katika bandari maalum za
nchi atakazotembelea, kwa ajili ya kukabiliana
na dharura yoyote ya kiafya ya Obama na familia
yake.

Ili kuwawezesha maofisa wa kijasusi wa
Marekani, ndege ya kijeshi ndiyo itakayobeba
magari 56 zikiwemo limousine 14 na magari
matatu maalumu ya kubeba mizigo.

Malori hayo yatakuwa yakibeba vioo ambavyo
ni vizuizi maalumu vya risasi na milipuko kwa
ajili ya kuongeza ulinzi kwenye hoteli
atakazolala yeye na familia yake.

Ndege za kivita kutawala anga
Ndege za kivita zitakuwa zikiruka kwa zamu
wakati wote muda wa sasa 24 kwa ajili ya
kuhakikisha ulinzi katika sehemu atakayokuwa
Rais Obama na kudhibiti anga yote kwa wakati
huo dhidi ya ndege yoyote ngeni itakatosogea
usawa wao.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na
Mwananchi, hakuna Maandalizi ya safari hiyo
ambayo tayari yamekamilika yanapolinganishwa na safari nyingine za aina hiyo zilizowahi kufanyika,
waraka maalumu kuhusu suala la usalama unaonesha kwamba kumekuwa na juhudi za ziada
zakuhakikisha ulinzi wa Amiri jeshi huyo Mkuu wa Marekani akiwa nje ya nchi.

Kabla ya safari yake kwa nchi za Afrika, Obama atatembelea Ireland na Ujerumani ikiwa ni sehemu ya
kuongeza changamoto inayokabili masuala ya usalama wake.

Lakini zaidi, safari ya Obama kwa nchi za Afrika inadhaniwa kuwa inayolazimisha waandaaji kuwa na
umakini wa hali ya juu na kuifanya iwe aghali zaidi katika utawala wa Obama kuliko ziara katika nchi za
ulaya, kwa mujibu wa wataalamu wa mipango.

Familia ya rais huyo inatarajiwa kutembelea nchi tatu za Afrika, ikiwemo Tanzania, Afrika Kusini na
Senagal kuanzia Juni 26 hadi Julai 3 mwaka huu.

Chanzo:Mwananchi.co.tz