Ajilipua na Moto Baada ya Kugomewa Kumuona PM

Kijana mmoja nchini Jordan
ambaye siku chache zilizopita
alikataliwa kuonana na Waziri wa
Ustawi wa Jamii wa Jordan na
kuamua kujiteketeza, amefariki
dunia hii leo kwenye hospitali ya
serikali mjini Amman.

Kijana huyo yatima aitwaye
Ahmad Rubain mwenye umri wa
miaka 23 ambaye siku ya Alhamisi
iliyopita alitaka kuonana na
Waziri wa Ustawi wa Jamii na
kumuelezea matatizo na hali
ngumu ya maisha inayomkabili,
aliamua kujiteketeza moto mbele
ya jengo la wizara hiyo baada ya
juhudi zake za kutaka kuonana na
waziri kugonga ukuta.

Msemaji wwa Hospitali ya serikali
ya al Bashir mjini Amman
amesema kuwa, asilimia 90 ya
mwili wa kijana huyo ilikuwa
imeteketea.

Hili ni tukio la tano
la kujichoma moto katika
kipindi cha miaka miwili nchini
humo.

Ni miaka miwili na nusu sasa
Jordan inakabiliwa na wimbi
kubwa la maandamano ya
wananchi wanaotaka yafanyike
marekebisho ya kisiasa, kiuchumi
na mapambano dhidi ya ufisadi
nchini humo.