Ngono Kinyume na Maumbile zaongezeka Tanzania

Taasisi ya Kupambana na Ukimwi
Nchini (Tacaids) imesema tafiti
mbalimbali zinaonyesha kuwa
vitendo vya ngono kinyume na
maumbile vinazidi kuongezeka.
Hayo yalisemwa jana na Dk.
William Kafura, katika mkutano
wa sita wa Chama cha Wabunge
cha Kupambana na Ukimwi
(Tapac).

Alisema hiyo inatokana na
imani za kishirikina kwamba
wakifanya vitendo hivyo
watapata bahati kwa
kupandishwa vyeo.

“Lazima tukubali tatizo lipo na
tulitafutie suluhisho, utafiti upo
umefanywa na Muhimbili,
umefanywa na chuo kikuu cha Dar
es Salaam, umefanywa na Tasisi ya
Utafiti ya Ifakara,” alisema.
Alisema pia wafanyabiashara
wanaamini kwa kufanya
vitendo hivyo watajirika wakati
wanawake wanaamini kuwa
watazidi kupendwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa
TACAIDS, Dk. Fatuma Mrisho,
alisema utafiti uliofanyika nchini
unabainisha kuwa wanawake
hawana uelewa wa kutosha juu ya
kujikinga na maambukizi ya
ukimwi.

Akizungumzia suala la kujikinga
na ugonjwa wa Ukimwi Dk. Mrisho
alisema kuwa wanaume wana
uelewa mkubwa zaidi kuhusu
ugonjwa huo kuliko
wanawake.Hata hivyo, alisema
kwa sasa ipo kazi kubwa ya kutoa
elimu kwa wananchi na hivyo
kuwataka wabunge na viongozi
mbalimbali kutoa elimu juu ya
kujikinga na gonjwa hatari la
ukimwi.

Aidha Mrisho alisema kuwa kwa
sasa Mkoa wa Njombe unaongoza
kwa maambukizi ya Virusi vya
ukimwi kwa asilimia 14.8 ambapo
Unguja Kaskazini inamaambukizi
madogo kwa asilimia 0.1.
Hata hivyo alisema kuwa kuna
changamoto mbalimbali ambazo
wanakumbana nazo ni pamoja na
rasilimali za ukimwi kwa serikali,
mashirika ya Dini na sekta binafsi
kuwa pungufu kuliko mahitaji.
Alisema pamoja na kuwepo kwa
changamoto lakini nia ni kufikia
sifuri tatu ifikapo mwaka 2015 na
hiyo hipo katika ulimwenguni,
Afrika hapa hapa Tanzania.