Kijana Anusurika kufa Kwa Kuchomwa Moto na Vibaka

Mtu mmoja aliyetambulika kwa
jina la Ismai Mayoba (31)
anayefanya kazi Bar ya
Mangrove, Mkazi wa Manispaa ya
Lindi amenusurika kifo baada ya
kuvamiwa na kundi la Vijana
waliotaka kumpora na hatimae
kumchoma moto.

Kwa sasa kijana huyo amelazwa
katika Hospital ya Sokoine Mjini
humo.

Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi
wilayani Lindi limefanikiwa
kumkamata mtu mmoja kati ya
watuhumiwa saba waliohusika na
tukio hilo lilitokea katika eneo la
Mtaa wa Congo.

Akithibitisha kuwepo kwa tukio
hilo na kukamatwa kwa
mtuhumiwa.

Afisa Mnadhimu wa
Jeshi la Polisi Mkoa wa
Lindi, Renatha Mzinga alimtaja
ndugu Ally Manially (22) mkazi wa
mtaa wa Kongo kuwa anashikiliwa
na Jeshi hilo na atafikishwa
mahakamani leo kujibu shitaka la
kujeruhi na kujipatia pesa kwa njia
ya Udanganyifu ikiwa pamoja na
kumchoma mwenzie Moto huku
akijua ni kosa kisheria.

Aidha Mzinga alieleza kuwa Jeshi
la polisi linaendelea kutafuta
watuhumiwa wengine 6
waliohusika na tukio hilo. Chanzo:Mpekuzi