Paul Kagame Aonesha Dharau Ushauri wa Kikwete

DHARAU za Rais wa Rwanda Paul
Kagame kwa Rais wa Jamhuri wa
Muungano wa Tanzania na Amiri
Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi
na Usalama Jakaya Mrisho Kikwete
zimewagawa Watanzania na
kuwafanya wawe na mitazamo
tofauti.

Wapo wanaomuunga mkono
Rais Kagame na wapo pia
wanaompinga kwa kauli yake...

Rais Kagame alimkejeli Rais
Kiwete kwa kuuita ushauri wake
ni ushauri wa kijinga kwa
wanyarandwa,awali Rais Kikwete
alizishauri nchi za Rwanda na
Congo DRC kukutana na kumaliza
tofauti zao kwa njia ya amani.

Rais Kikwete alitoa ushauri huo
wakati wa mkutano wa kujadili
amani na mpango wa ulinzi nchini
Congo DRC uliofanyika katika
Makao Makuu ya AU mjini Addis
Ababa Ethiopia.

Katika ushauri huo Rais Kikwete
alisema kwamba ni vyema Rais
Kagame akakaa katika meza ya
mazungumzo ya amani na Rais wa
Congo DRC Joseph Kabila ili
kumaliza tofauti zao badala ya
kutumia nguvu ya kijeshi.

"Nimekaa kimya kwa kipindi
kirefu na kwa jinsi nilivyoweza
kwa sababu nilifikiri kwamba
mazungumzo ya kipuuzi
yaliyozungumzwa na watu
wajinga yamemalizika "alisema
Rais Kagame.

Katika hatua nyingine Rais Kagame
alisema kwamba ushauri huo wa
Rais Kikwete ni sawa na
kuwachezea wanyarandwa mbele
ya mataifa.

Rais Kagame aliyasema hayo
katika sherehe ya kuhitimu
mafunzo ya maofisa wa jeshi
wapatao 45 katika kituo cha
mafunzo ya kijeshi siku ya Juma
Tatu nchini Rwanda.


NB:
RAIS WETU SIYO MJINGA...
HILO NI TUSI , JK ALIWAPA
USHAURI WA BURE...MLIKUWA
HURU KUUTUMIA AU KUUACHA