Ivory Coast Watwangana

Wachezaji wawili wa Ivory Coast
wametimuliwa kwenye kikosi
kinachojiandaa na mchezo kuwania
kufuzu michuano ya kombe la dunia
mwaka 2014 dhidi ya Tanzania
unaotarajiwa kupigwa uwanja wa
Taifa siku ya Jumapili.

Mchezaji wa zamani wa Monaco
Jean-Jacques Gosso Gosso, 30,
ambaye kwa sasa anakipiga kwenye
ligi ya Uturuki akiichezea Mersin na
kinda la miaka 20 Abdul Razack wa
Manchester City, ambaye kwa sasa
yupo kwa mkopo Charlton Athletic,
walipigana siku ya jumatano wakati
timu yao ikiwa kwenye maandalizi ya
mwisho kabla ya kuja Tanzania usiku
wa leo.

FA ya Cote D'Ivoire imesema
kwamba adhabu nyingine zinaweza
kufuatiwa kutegemea na kamati ya
nidhamu itakavyoamua.

Wakati huo huo timu hiyo ya Ivory
Coast imeshafika nchini na
wamefikia kwenye hoteli ya Bahari
Beach.