Mzee Aboud Jumbe afikisha miaka 93

Imeelezwa kuwa moja kati ya
neema alizopewa
mwanaadamu ni umri mrefu
hivyo ni wajibu wa kila mmoja
wetu kuutumia vyema uhai
wake kwa kutenda mema na
kushukuru kila siku kwani
hapaswi mwanaadamu kuwa
aasi bali anachotakiwa ni
kumuabudu Mola wake
aliyemuumba.

Kadhi mkuu wa Zanzibar
Sheikh Khamis Haji Khamis
ameyasema hayo katika dua ya
kumshukuru Mwenyezi Mungu
kutimiza miaka 93 ya kuzaliwa
kwa Rais Mstaafu wa Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar Alhajj
Aboud Jumbe Mwinyi
iliyofanyika Kiembe Samaki.

Sheikh Khamis Haji ametowa
ukumbusho kwa kusema kuwa
“ Ifanye dunia kama kwamba
utaishi milele kwa maana ya
kutenda mazuri na kumuabudu
Allah kama tulivyoamrishwa
katika dini pia ifanye akhera
yako kama utakufa sasa kwa
maana ya kujiandaa kwa
kutenda amali njema na
kuomba msamaha kila siku.

Katika khutba yake iliyosomwa
na Ustadh Moh’d Yoyota kwa
niaba yake Rais Mstaafu
Awamu ya Pili Alhajj Aboud
Jumbe amesema kuwa
anamshukuru Mola wake kwa
umri aliyomjaalia kwani
ameshuhudia neema nyingi
ambazo hazina kiima kisicho
kifani,kina wala mizani katika
maisha yake na kupitia nyanja
tofauti za maisha hadi M/
Mungu atakapomjaalia mwisho
wa maisha yake.

Alhajj Aboud Jumbe ameongeza
kusema kuwa anamshukuru
Mola wake kwa kumpa rehema
zake huruma na hisani pale
alipokabidhiwa dhamana ya
kuongoza baadae kumnusuru
na kumfariji na hatimae
kumuongoza pale alipoteleza
mnamo asiyoyaridhia kwani
majibu sahihi ya mithani yetu
wanaadamu yanasubiri siku
ya malipo ambayo yatupasa
tutambue kuwa kila mmoja
wetu atakutana nayo.

“Namuomba Mwenyezi Mungu
kwa unyenyekevu azidi
kuitakasa amali yangu na
kunipa khusni l khatima mimi
pamoja na waislamu wenzangu

Akitowa shukurani kwa
waalikwa waliohudhuria
katika dua hiyo kwa niaba ya
familia ndugu Mustafa Aboud
Jumbe ambae ni mtoto wake
amesema kuwa lengo la
kusoma dua hii ni
kukumbushana namna gani
tunatumia neema na kila
mmoja vipi atautumia uhai
wake na kusisitiza kuwa dua
hio ni mwenyewe baba yao
aliyetowa utaratibu juu ya
namna gani isomwe dua hio
“Tumekuwa tukipata masuala
mengi kuhusu hali ya mzee
wetu jibu ni kwamba hajambo
ila uzee tu ndio unaomsumbua,
nuru ya macho
imepotea ,kusikia kumekuwa
shida kidogo lakini anasikia
na anazungumza na hii
shughuli yake ya leo amepanga
mwenyewe”alisisitiza Mustafa
Jumbe.

Nae Sheikh Moh’d Iddi
ametowa wito kwa jamii
kufanya matendo mema kwani
kuwepo kwetu ipo historia
ambayo M/ Mungu
amewashushia waja wake na
aliyebahatika kuishi kwa
kumuabudu huyo atakuwa
amefaulu.
Miongoni mwa waliohudhuria
katika dua hio ni pamoja na
Kadhi Mkuu Mstaafu Sheikh
Habib Ali Kombo baadhi ya
Masheikh, Familia yake,
baadhi ya wanafunzi aliwahi
kuwasomesha na
kuwafundisha kazi

Chanzo:IssaMichuzi