Katavi Warriors Wakubali Kwata

Timu ya soka mabingwa na kiboko wa timu za Saigon na Rukwa United, Katavi Warriors kutoka mkoani Katavi Wamekubali kupiga kwata kutoka kwa Polisi Jamii ya mkoani Mara kwa goli mbili bila (2-0).

Katavi walikubali kichapo hicho katika kipindi cha pili cha mchezo huo. Kutokana na kufungwa huko Katavi wataitaji ushindi wa goli 3 kwa bila ili kuweza kufuzu kwa round inayofuata.

Mchezo wa marudiano unatalajia kufanyika baada ya wiki moja katika uwanja wa Azimio ambao umekuwa mgumu sana kwa timu za ugenini kuibuka na ushindi.

Aston Villa kama inavyofahamika katika mita ya Majengo, Makanyagio, kawajense na viunga vyote vya Nsemula na mpanda kwa ujumla. Wameingia katika hatua hiyo baada ya kuwaondosha Rukwa United kutoka Sumbawanga mkoani Rukwa na Saigon Fc kutoka Kigoma.

Timu zote zinashiriki ligi ya TFF ngazi ya mtoa ili kufuzu na kuingia ligi kuu. Kila la heri kwa Katavi Warriors katika mchezo wa marudiano.