Polisi Jamii waendeleza Kwata kwa Katavi Warriors

Timu ya Polisi jamii kutoka Mkoani mara wilayani Bunda imeendeleza ubabe kwa Katavi Warriors Kutoka Mkoani katavi baada kufanikiwa kuibuka na ushindi katika michezo yake iliyopigwa nyumbani na ugenini katika ligi ya Tff hatua ya mtoano.

 Mchezo wa kwanza ulifanyika mkoani mara ambapo Katavi walikubali kichapo cha goli mbili kwa nunge. Mchezo huo uliwaweka Katavi katika mazingira magumu ambapo waliitaji ushindi wa Goli tatu bila ili kuwezesha kufuzu round inayofuata.
Polisi jamii wakishangilia
  
 Katika mchezo wa leo(Alhamisi 21 june) ulioanza kupigwa majila ya saa kumi na nusu jioni. Katavi warriors walikuwa wanahitaji ushindi wa kuanzia goli mbili, ambapo walifanikiwa kupata ushindi huo na kufanya matokeo ya jumla kusomeka (2-2), magoli hayo yaliyopachikwa kipindi cha pili cha mchezo yaliwezesha mchezo kuingia katika hatua ya kupigia penati. Ambapo walikuwa ni Polisi walioanza kupiga penati hizo.
 Ambapo piga nikupige ya penati zote tano ilikamilika kwa kila timu kuwa imepata penati 4 ya 5 ambapo iliongezwa moja kila upande, 

Walikuwa ni Polisi walioweza kutumia nafasi hiyo vizuri na kuweza kufunga, huku Mcheza wa Katavi Emmanuel akishindwa kutupia mpira kambani. kwa kipa wa Polisi kuicheza penalty kwa ustadi kama inavyoonekana pichani chini.
Kipa Akicheza Penati ya Mwisho
 Hiyo ndiyo ilikuwa safari ya mwisho ya wana katavi kuweza kusonga mbele. katika michuano hiyo ya TFF ngazi ya mtoano. Katavi mpaka kufikia hapo waliziondosha timya Ya Rukwa United na Saigon Fc kutoka mjini kigoma.

Kocha wa Katavi Warriors
Katavi wamekuwa wazuri katika uwanja wa Nyumbani Azimio, kwa kutoruhusu kushindwa katika uwanja huo. Hakika Polisi jamii wavunja rekodi hiyo kwa kuchomoza na ushindi katika uwanja huo.

Wachezaji wa Katavi wakiwa na huzuni.


Kocha Mkuu wa Polisi Jamii

Polisi Jamii wakishangilia
Mashabiki waliofulika kuja kuangalia mechi

Baada ya Mechi

                                Tazama jinsi polisi jamii walivyokuwa wakishangilia ushindi huo


Kila la heri Polisi jamii huko mbele ya safari, na Maandalizi mema kwa Katavi Warriors(AstonVilla) kwa ajili ya Ligi msimu ujao.