Mtikila: Nitakwenda kwenye mahakama za Kimataifa

Mchungaji Dr. Christopher Mtikila amesema atakwenda kwenyd mahaka za kimataifa kupinga rasimu ya katiba mpya kwa kutoitambua Tanganyika.

Ikiwa zimepita siku chache tu tangu kuzinduliwa kwa rasimu ya katiba mpya Mtikila amesema atakwenda hata kwenye mahakama za kimataifa kupinga Rasimu hiyo kwa kutoitambua Tanganyika ambapo katika rasimu hiyo kumependekezwa serikali tatu Zanzibar, Serikali ya shirikisho na Tanzania Bara.

Dr. Mtikila anapinga uwepo wa Tanzania bara Badala ya Tanganyika.