Mtoto Wa Michael Jackson Ajaribu Kujiua

Bintiye marehemu Michael Jackson,
Paris, mwenye unmri wa miaka 15,
amelazwa katika hospitali moja mjini
Carlifornia baada ya kujaribu kujiua.

Msemaji wa familia ameeleza kuwa
anaendelea kupata nafuu na kuwa
madaktari wanamshughulikia vilivyo.

Inasemekana, Paris Jackson, ambaye
babake alifariki mwaka 2009,
amekuwa katika hali ya kusononeka
kwa muda sasa.

Msemaji wa familia hiyo amesema
kuwa usiku wa kuamkia leo binti huyo
alikimbizwa hospitalini baada ya
kujaribu kujiua lakini anaendelea
kupata nafuu.

Msemaji alifafanua kuwa hali yake si
mbaya sana ya kupelekwa kwa wadi
ya wagonjwa mahututi.

Paris Jackson ametajwa kama mmoja
wa familia ya Michael Jackson
anayetaka kulipwa mamilioni ya Dolar
kutoka kampuni ya AEG ambayo
ilimwajiri daktari aliyempa madawa
Michael ambayo yaligunduliwa
baadaye kuwa yalimwua.
Kesi inayohusiana na madai hayo
imeendelea kwa majuma sita sasa.

Mengi ya kusikitisha juu ya Michael
Jackson yamekuwa yakitajwa na
inadhaniwa kwamba yamechangia
pakubwa kupandisha huzuni na
simanzi kwa msichana Paris.

Inadhaniwa kuwa Paris amejaribu
kadiri ya uwezo wake kumwomboleza
baba yake lakini angali anasononeka
kutokuwepo kwake.

Mlezi wake
kisheria ni nyanya yake Catherine
lakini hata hivyo siku chache zilizopita
amekuwa akiishi na mamake mzazi.