Misri Watoa Onyo kwa Ethiopia

Rais wa Misri Mohammed Morsi
amesema kuwa taifa lake litatumia kila
mbinu kuhakikisha kuwa Ethiopia
inasitisha ujenzi wa bwawa la maji
katika mto Nile.

Idadi kubwa ya raia wa Misri millioni
84 imekuwa ikitegemea mto huo kwa
maji safi.

Akishangiliwa na wafuasi wake ,Morsi
amesema kuwa ijapokuwa Misri
haitaki vita haitokubali usalama wake
wa maji kuingiliwa kivyovyote.

Tayari kiongozi huyo anapanga
kumtuma waziri wake wa maswala ya
kigeni nchini Ethiopia ili kuanzisha
mazungumzo kuhusiana na swala
hilo.

Misri ina wasiwasi kuwa maji ya mto
Nile huenda yakapungua kwa kiwango
kikubwa iwapo bwawa hilo litajengwa.

Inasema kuwa, kwa mujibu wa sheria
zilizowekwa na mkoloni, ndio taifa
linalopaswa kufaidika pakubwa na
maji hayo swala linalopingwa na
Ethiopia ambayo inasema sheria hiyo
imepitwa na wakati.