WATOTO WAFUNGIWA NDANI TANGU KUZALIWA KWAO.

Polisi nchini Ghana wanawahoji
wazazi walioshtakiwa kwa kuwafungia
nyumbani wanao walio kati ya umri
wa miaka minne na minane tangu
kuzaliwa kwao.

Polisi walivamia makao yao yenye
vyumba vinne mjini Accra, siku ya
Ijumaa na kuwaokoa watoto hao,
mvulana mmoja na wasichana wawili.

Wazazi hao waliwaambia polisi kuwa
hawakutaka kuwatoa wanao nje kwa
hofu ya kukusanyika na watu waovu.

Watoto hao sasa wamepelekwa katika
makao ya kuwatunza watoto huku
kukiwa na hofu kuwa wazazi wao
huenda ni wagonjwa wa akili.

Mwandishi wa BBC mjini Accra
anasema kuwa kisa hicho
kimewashangaza sana watu mjini
humo.

Inaarifiwa watoto hao walifungiwa
nyumbani tangu kuzaliwa kwao na
hawamkujua yeyote isipokuwa wazazi
wao.

Aidha watoto hao waliishi katika
chumba kimoja, huku Kondoo na
kuku wakiwa katika vyumba viwili
huku wazazi wao wakilala katika
chumba chao kwenye nyumba hiyo
iliyikuwa imejaa uvundo.
Nyumba ilionekana kama isiyoishi
watu na licha ya kuwa haikuwa
imesafishwa kwa miaka mingi, kuta
zake zilikuwa na michoro.
Polisi walivamia nyumba hiyo baada
ya jirani mmoja mwenye shauku
kuwaarifu.

Wazazi wa watoto hao wanahojiwa na
polisi pamoja na madaktari wa
magonjwa ya kiakili mjini Accra, huku
watoto hao wakipewa malezi na
familia moja.

Msemaji wa polisi alisema kuwa
wazazi wa watoto hao hawakuwahi
kuruhusiwa kutoka nje ya nyumba
yao.

Watoto waliwaarifu polisi kuwa baba
yao ambaye hakuwa na ajira,
aliwasomesha hesabu na kiingereza
nyumbani kwao.

Chanzo:BBC