MBAKAJI SUGU WA SOUTH AFRIKA AFARIKI

Mwanamume anayetuhumiwa kuwa
mbakaji sugu nchini Afrika
Kusini ,Sifiso Makhubo, amepatikana
akiwa amefariki katika chumba chake
gerezani.


Sifiso Makhubo, aliyekuwa anakabiliwa
na mashtaka 122 ikiwemo mauaji na
ubakaji alipatikana akiwa amejinyonga
kwa blanketi.


Baadhi ya makosa aliyoshtakiwa nayo
ni pamoja na kuwaambukiza
waathiriwa virusi vya HIV
Afrika Kusini ina moja ya visa vingi
zaidi vya ubakaji duniani, huku polisi
wakionyesha kuwa ni visa 64,000
pekee ambavyo viliripotiwa mwaka
jana.


Maafisa wanasema kuwa alikuwa peke
yake katika seli yake , lakini
wanachunguza kilichosababisha kifo
chake.


Bwana Makhubo anatuhumiwa kwa
kuwabaka watoto 35 na wanawake
wawili, kati ya Januari mwaka 2006 na
Februari 2011.


Hadi sasa uchunguzi uliofanywa wa
DNA katika waathiriwa waliodai
kubakwa naye, ulithibitisha kuwa yeye
ndiye alikuwa mbakaji.

Source:BBC