MWANAFUNZI WA IFM AFIA BAHARI YA HINDI

Mwanafunzi wa Mwaka wa
Kwanza Uhandisi wa Kompyuta
wa chuo cha Usimamizi wa Fedha
(IFM) Wendy Habakuki Lwendo
amefariki dunia katika ufukwe wa
bahari ya Hindi eneo la Kipepeo
Kigamboni akiogelea na wenzake
watatu jana jioni.


Taarifa kutoka kwa kaka wa
Marehemu, Sammy Lwendo
amesema mdogo wao alipatwa na
masaibu hayo akiwa na rafiki zake
hao watatu wakiogelea baharini na
wakati wanaogelea walikuwa
katika eneo la kina kifupi cha maji
yaliyokupwa na mara maji hayo
yaka jaa na walipokuwa
wakijaribu kutoka ndipo Wendy
akazidiwa na maji.


Lwendo amesema kuwa wenzake
walifanikiwa kumtoa majini lakini
hali yake tayari ilikuwa mbaya na
kwakuwa hawakuwa na ujuzi wa
kutosha wa kutoa huduma ya
kwanza kwa mtu
aliyezama majini walihangaika
kwa zaidi ya dakika 40 kumsaidia
ndipo wakapata msaada wa
Polisi kumkimbiza kituo cha afya
Kibaoni huko Kigamboni lakini
jitihada za kuokoa maisha yake
ziligonga mwamba.


Aidha alisema kuwa mwili wa
Marehemu ulihamishiwa katika
Hospitali ya Wilaya Vijibweni na
sasa ndugu wamefika na
kuhamishia mwili huo Hospitali ya
jeshi Lugalo.


Msiba kwa sasa upo Kinondoni
nyuma ya Vijana, huku
wakisubiriwa wazazi wa
marehemu pamoja na ndugu
wengine ili kujua taratibu kamili
za maziko.


Wazazi wa Wendy, Mchungaji
Habakuki Lwendo ni mwalimu wa
Chuo cha Uchungaji Makumira
mkoani Arusha.