KOCHA WA ZAMANI WA TAIFA STARS AFARIKI.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) limepokea kwa masikitiko
taarifa za kifo cha kocha wa zamani wa
Taifa Stars, Bert Trautmann (89)
kilichotokea jana (Julai 19 mwaka huu)
nchini Hispania.


Kabla ya kuwa kocha, Trautmann
aliyezaliwa 1923 mjini Bremen,
Ujerumani
alikuwa kipa wa timu ya Manchester
City ya Uingereza ambapo
anakumbukwa kwa
kucheza mechi ya fainali ya Kombe la
FA dhidi ya Birmingham City akiwa
amevunjika shingo.

Manchester City ilishinda fainali hiyo
iliyochezwa mwaka 1956 mabao 3-1.


Trautmann ambaye aligongana na
mshambuliaji wa Birmingham, Peter
Murphy
zikiwa zimesalia dakika 17 mechi hiyo
kumalizika aligundua kuwa amevunjika
shingo siku tatu baadaye.


Mbali ya kuwa kocha wa Taifa Stars
mwanzoni mwa miaka ya 60,
Trautmann pia
alikuwa mkufunzi wa makocha
ambapo hapa nchini aliendesha kozi
mbalimbali
zilizotoa makocha waliokuja kutamba
baadaye.


TFF itamkumbuka Trautmann kwa
mchango wake aliotoa katika
maendeleo ya
mpira wa miguu nchini ikiwemo wazo
lake la kuanzishwa kwa Ligi Kuu (Daraja
la Kwanza) ambalo alilitekeleza katikati
ya miaka ya 60.


Msiba huo ni pigo kwa familia ya
Trautmann, TFF na familia ya mpira wa
miguu kwa ujumla nchini kutokana na
mchango alioutoa kwa Tanzania hasa
wakati akiwa kocha na mkufunzi wa
makocha.


TFF inatoa pole kwa familia ya
marehemu Trautmann, Chama cha
Mpira wa Miguu
cha Ujerumani (DFB), Chama cha
Mpira wa Miguu cha Uingereza (FA) na
kuwataka kuwa na uvumilivu katika
kipindi hiki cha msiba huo mzito.


Mungu aiweke roho ya marehemu Bert
Trautmann mahali pema peponi.