Morsi Apinduliwa Misri

jeshi nchini Misri limemuondoa
madarakani Rais aliyechaguliwa kwa
njia ya kidemokrasia nchini humo
Mohamed Morsi na imemteuwa
kiongozi wa muda wa nchi baada ya
maandamano makubwa
yanayoipinga serikali.

Akihutubia kwa njia ya televisheni
jumatano jioni, mkuu wa jeshi,
Abdul Fatah Khalil Al-Sisi alisema
katiba ya Misri imesitishwa kwa
muda na mkuu wa mahakama ya
katiba ameteuliwa kuwa kiongozi wa
muda nchini humo.

Sisi alitangaza kwamba jeshi
linaangalia watu wa Misri kufuatana
na maandamano makubwa ya
upinzani yakidai kuwa Rais
Mohamed Morsi ajiuzulu.

Kufuatia hotuba ya kwenye
televisheni Bwana Morsi alitoa
taarifa kupitia akaunti yake ya
Twitter, akiita hatua ya jeshi ni
"mapinduzi kamili".

Aliwasihi wa-
misri wote kukataa hatua ya jeshi
lakini pia aliwataka kuwa na amani.

Kiongozi mpya wa muda nchini
Misri, Adli Mansour ana umri wa
miaka 68 ni mkuu wa sheria katika
mahakama ya juu ya katiba.

Ataapishwa alhamisi.

Kama sehemu ya mwongozo mpya
unaoungwa mkono na jeshi kwa
nchi, sisi aliutaka uchaguzi wa urais
na wabunge, jopo kutathmini katiba
na kamati ya mashauriano kitaifa.

Alisema mwongozo ulikubaliwa na
makundi kadhaa ya kisiasa.

Pia aliwasihi watu wa Misri
kuepukana na ghasia. Jeshi lilimpa
Bwana Morsi saa 48 kutatua
matatizo ya kisiasa au kuwepo hatari
ya jeshi kuingilia kati.

Viongozi wa jeshi walisema
wataweka "mwongozo" kama
tofauti kati ya serikali ya ki-islam na
wapinzani wake hawatamaliza
matatizo yao ifikapo jumatano
mchana ya tarehe tatu mwezi wa
saba mwaka 2013. Tarehe hiyo ya
mwisho ilipita muda wake bila ya
hatua zozote kuonekana.

Bwana Morsi hakika alikataa wito wa
kujiuzulu na aliapa kuendelea
kubaki madarakani hata kama
itamsababishia kifo chake.

Pia
alilalamika jeshi kutoa kitisho chake
cha kuingilia kati katika matatizo ya
kisiasa.

Baruti zilipaa angani kwenye umati
wa watu wanaocheza na
kupeperusha bendera katika uwanja
wa tahriri Square mjini cairo, kiini
cha ghasia za mwaka 2011 ambazo
zilimuondoa Rais wa muda mrefu
nchini Misri, Hosni Mubarak.

Katika wiki ilizopita maandamano
yenye ghasia kati ya wafuasi na
wapinzani wa bwana Morsi
yameuwa takribani watu 40.

Jeshi la Misri limetangaza kuchukua
madaraka ya nchi hiyo huku
likitangaza kuwa si mapinduzi lakini
Mohamed Morsi si rais tena wa
Misri. Tayari Saudia Arabia imetuma
salamu za pongezi kwa mkuu wa
jeshi la nchi hiyo kwa kuchukua
madaraka.

Hali ya rais Morsi ilikuwa ngumu
pale wananchi wake walipoamua
kuingia mitaani kumpinga siku
chche zilizopita kwa maandamano
baada ya kujitwalia madaraka mengi
kiutawala kama mtangulizi wake.