MBUGE WA CCM AHUSISHWA NA USAFIRISHAJI DAWA ZA KULEVYA

Ni jambo la wazi wamba biashara
ya madawa ya kuleya ni biashara
ambayo mara nyingi hubebwa na
watu wenye nazo au wenye
madaraka fulani makubwa.
Ni
biashara ambayo ina faida kubwa
na ya haraka pengine kupita aina
nyingine yeyote ya biashara (halali
na haramu).

Na kutokana na nguvu ya vyombo
mbalimbali vya dola ulimwenguni
katika kupambana na biashara hii,
ni wazi kwamba bila kuwepo na
connection za hali ya
juu,utekelezaji wa biashara hii
ungekuwa mgumu sana…
Ndio maana vita dhidi ya biashara
hii haramu ni ngumu na ambayo
inahitaji umakini wa hali ya juu
zaidi katika kukabiliana nayo
endapo kuna nia ya dhati ya
kuitokomeza au japo kuipunguza.

Hivyo basi,haishangazi sana
(japokuwa hizi ni tuhuma tu)
kusikia yale yaliyotajwa katika
“barua kutoka Hong Kong” kwa
miongoni mwa watanzania
wanaosemekana kufikia hata 200
wanaosota katika jela za nchini
humo  kusikia majina ya watu
waliotajwa katika waraka huo
ambao bila shaka utapamba
vyombo mbalimbali vya habari
nchini Tanzania wiki kadhaa
zijazo.

Kutajwa kwa wazi wazi kwa
majina ya baadhi ya
wanaotuhumiwa kuhusika na
huku mwandishi wa barua hiyo
akionya kwamba majina mengine
zaidi yapo, kunaifanya barua hiyo
kuwa tofauti kabisa na barua za
kawaida au hata zile tambo za
kisiasa kwamba “wanaohusika na
biashara hii nawajua”
Miongoni mwa majina hayo, limo
jina la Mbunge wa Jimbo la
Kinondoni kwa tiketi ya CCM, Iddi
Azan.

Barua hiyo (ambayo utaisoma
hapa chini) inahitaji kufanyiwa
uchunguzi wa kina. Lakini
kutokana na ukweli kwamba
imeainisha watu wanaosadikiwa
kuhusika, bila shaka imelipa jeshi
la polisi mahali pazuri pa kuanzia.

Je,wanaotajwa kipato chao
kinatokana na biashara gani zilizo
halali? Ukaguzi wa vitabu vyao
vya fedha unasemaje?
Jambo moja ambalo linasikitisha
sana (endapo tuhuma hizi
zitathibitishwa hususani kumhusu
Iddi Azan) ni kwamba Jimbo au
Wilaya ya Kinondoni ni miongoni
mwa maeneo ambayo yanaongoza
kwa vijana kuathirika na matumizi
ya madawa ya kulevya.

Je,ina
maana Mbunge wake anahusika
katika kuangamiza vijana au
wapiga kura wa jimbo lake
mwenyewe?

Pitia link hii kujua zaidi www.v2catholic.com/johnw/2013/2013-07-21drug-mules.htm

SOMA BARUA YENYEWE HAPA
CHINI…