Bus La Sumry Lapata Ajari Tena.

Kampuni ya mabasi ya sumry imeendelea kukubwa na balaa baada ya Bus jingine tena la kampuni hiyo kupata ajari hivi leo katika maeneo ya mbuga nyeupe ndani ya hifadhi ya taifa ya Katavi, Mkoani Katavi.

Ajari hii imetokea ikiwa ni wiki moja tu baada ya bus jingine la kampuni hiyo ya Sumry kutumbukiakatika Mto Katuma eneo la Stalike nje kidogo hifadhi ya Katavi ambapo walifariki watu tisa na majeruhi 53.

Katika ajari ya hivi leo iliyotokea majira ya mchana kwa bus lililokuwa linatoka Mpanda kuelekea Sumbawanga kupinduka, hakuna mtu aliyefariki ni majeruhi tu.

Baadhi ya majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Mpanda, na wengine kuendelea na safari kwa kufuatwa na bus jingine. Mungu awatie nguvu majeruhi wote.