Bus La Sumry Lapata Ajari Lauwa na Kujeruhi

Kwa habari zilizotufikia ni kuwa bus la kampuni ya sumry limepata ajari katika eneo la Stalike Mkoani Katavi.

Bus hilo lilikuwa linatoka mkoani Mbeya kuja Mpanda Katavi, Ajari hiyo imetokea majira ya saa sita usiku ambapo shuhuda mmoja amesema kuwa ajari imetokea baada ya bus kufail break na Kupitiliza katika mto katuma ulipo katika eneo hilo na ni maarufu kwa kuwa na viboko wengi.

Pia ameongezea kwa kusema kuwa alishuhudia maiti ya mtoto ikitolewa, pia mmoja wa askari wa wanyama pori wa hifadhi ya taifa ya katavi amesema kuwa kampuni ya kutengeneza barabara inayofanya kazi katika maeneo hayo wamesaidia kulitoa bus mtoni ambapo maiti wanne wamepatikana na kufanya idadi ya maiti kufikia tisa pia ameongezea kwa kusema inawezekana kukawa na maiti zaidi ndani ya mto huo na pia kuna majeruhi wasiopungua 30.

Watu wamefulika katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda kuangalia majeruhi. Tunatoa pole kwa wafiwa na Mungu awatie nguvu na kuwaponya majeruhi wote.

Tutawapatia habari kama zitakavyokuwa zikipatikana.