Waathirika Wa Shambulio 1998 Wakumbukwa

Rais wa Marekani Barack Obama
ameweka mauwa kwenye makaburi ya
waathiriwa wa mashambulizi ya
mabomu dhidi ya ubalozi wa
Marekani nchini Tanzania mwaka
1998, kama ishara ya kuwakumbuka.
Raia 11 wamarekani waliuawa katika
shambulizi hilo lililofanywa na kundi
la kigaidi la al-Qaeda ambaklo
lilifanyika wakati mmoja na shambulizi
lililofanywa dhidi ya ubalozi wa
Marekani mjini Nairobi, Kenya.

Obama aliuungana na rais mstaafu
wa Marekani George W Bush kwa
kumbukumbu hizo.

Rais Obama yuko katika mkondo wa
mwisho wa ziara yake ya pili ya Afrika
akiwa rais , ambapo alitembelea
Senegal na Afrika Kusini.

Aidha Obama pia atamtembelea kituo
cha kuzalishha umeme
kinachomilikiwa na Marekani nchini
humo, kufuatia tangazo lake
mwishoni mwa wiki la mradi wa
umeme utakaogharimu mabilioni ya
dola.

Mradi huo wa miaka mitano,
unatarajiwa kusaidia kuongeza kasi ya
uzalishaji wa umeme kusini mwa
jangwa la Sahara,kwa ushirikiano na
mataifa ya kiafrika pamoja na sekta
binafsi.

Akiwa nchini humo, Obama pia
anatarajiwa kuzindua mpango
unaonuia kusaidia nchi za Afrika
Mashariki ikiwemo, Burundi, Kenya,
Rwanda, Tanzania na Uganda
kushirikiana kibiashara.

Wakati huohuo, mkewe Obama,
Michelle anatarajiwa kuhudhuria
mkutano wa wake za marais,
unaoandaliwa na taasisi ya George W
Bush huku ukiongozwa na mkewe
Laura Bush.