MKOJO WATUMIKA KUOTESHEA MENO

Wanasayansi wamekuza jino kutoka kwa mkojo wa
binadamu
Matokeo haya yaliyochapishwa kwenye jarida la
utafiti wa kisayansi la Cell Regeneration,
yalionyesha kuwa mkojo unaweza kutumika
kuunda celi ambazo zinaweza kutumika kukuza
vimelea vinavyofanana kama meno.


Wanasayansi kutoka China waliofanya utafiti huo
wanatumai kuwa utafiti huu unaweza kutumika
kuwapa watu wasio na meno fursa ya kuwa nayo.
Hata hivyo watafiti wa celi za mwili, wanaonya
kuwa utafiti huu unakabiliwa na changamoto
nyingi.


Vikundi vya wanasayansi kote duniani wanatafuta
mbinu za kukuza meno kwa njia ya mahabara ili
kukabiliana na tatizo la wazee kung'oka meno na
hata wale wanaong'oka meno kutokana na afya
mbaya.

Seli zijulikanazo kama -Stem cells - ambazo
wanasayansi wanaweza kutumia kukuza aina
yoyote ya seli, hutumika sana katika sekta ya utafiti.


Wanasayansi wa China waliofanya utafiti huo,
walitumia mkojo wa binadamu, mwanzoni mwa
utafiti wao.


Seli zinatoka mwilini kwa njia ya mkojo ,
zilikusanywa na kuwekwa kwenye
mahabara.Mchanganyiko wa seli hizi na zile
zilizokusanywa kutoka kwa panya ambao hutumiwa
kwa utafiti, ziliwekwa ndani ya mwili wa Panya.


Baada ya wiki tatu seli hizo zilianza kufanana kama
meno zikiwa na sehemu zote za jino. Hata hivyo
meno yenyewe hayakuwa magumu kama meno ya
kawaida.

Utafiti huu hata hivyo unahitaji kazi ya ziada ili
kuzalisha meno halisi.


Profesa Chris Mason, mwansayansi wa seli za
mwili, alisema kuwa mkojo wa binadamu sio hatua
nzuri ya kuanzia kutengeza meno halisi.


Sio kiungo kizuri kutumia kwa sababu mkojo hauna
seli nyingi na kazi ya kugeuza mkojo kuwa seli ni
ngumu sana.


Pia alionya kuhusu tisho la maambukizi kutokana
na viini vya bakteria vilivyo kwenye mkojo.

Chanzo:BBC