AMUUWA MKEWE KWA KISU


Jeshi la polisi  Mkoa wa Katavi linamsaka
Dickson Petro mkazi wa Kijiji cha Mwamkulu
Kata ya Kakese wilaya ya Mpanda  kwa tuhuma
za kumuuwa mke wake kwa kumkata na kitu
chenye ncha kali  kichwani .usoni,na kwenye
mikono yake yote baada ya mwanamke huyo
kukataa kuishi na mumewe.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Katavi Dhahiri
Kidavashari alimtaja mwanamke aliye uwawa
na mumewe kuwa ni Solile Elikana (35) mkazi
wa kijiji hicho cha Mwamkulu tukio hilo la
mauwaji ambalo lilitokea hapo julai 15 mwaka
huu majira ya saa nne usiku nyumbani kwa
marehemu.

Alisema chanzo cha kifo cha  mwanamke huyo
kilitoka na ugomvi wa wanandoa hao hao
wawili  uliotokea hapo  julai 12 mwaka huu na
kusababisha mwanamke huyo kukataa kuishi
na mumewe mbele ya kikao cha baraza la
serikali ya kitongoji cha Mwamkulu.

Marehumu huyo aliamua kumshitaki mumewe
kwenye baraza hilo la serikali ya kijiji baada ya
mumewe  kumpiga na kumsababishia majeraha
sehemu ta uso wake  kitendo ambacho
kilimuudhi marehemu  baada mumewe
kumtuhumu mkewe kuwa ana mahusiano ya
kimapenzi na mwanaume mwingine kijijini
hapo.

Alisema baada ya mwanaume huyo
kushitakiwa kwenye baraza hilo  aliamua
kwenda kwa mwenyekiti wa kitongoji aitwaye
Laulian Ngalu ili aweze  kuwasululisha lakini
marehemu alikataa  hari ambayo ilimfanya
mwenyekiti  huyo aitishe kikao cha serikali ya
kitongoji  kwa lengo la kuendelea
kuwapatanisha.

Hata hivyo katika kikao hicho marehemu
alikataa kata kata kuendelea kuishi na
mumewe na kisha aliamua kwenda kuchukua
nguo zake na vyombo vyote walivyo nunua na
mume wake waligawana licha  ya mume
kumwomba marehemu waedelee kuishi
pamoja  lakini marehemu aligoma.

Kidavashari alieleza kuwa  baada ya kugawana
vyombo hivyo mtuhumiwa akuonekana tena
kijijini hapo kwa muda wa siku tatu toka
walivyo achana na marehemu.

Alieleza kuwa  ndipo siku hiyo   alipo onekana
mtuhumiwa Dickson palikuwa na mkesha wa
harusi kijijini hapo na marehemu  ni miongoni
mwa walioshiriki sherehe hiyo
kamanda Kidavashari  alieleza ndipo ilipo
ilipotimia majira ya saa nne usiku marehemu
aliamua kurudi nyumbani kwake  na alipo fika
karibu na nyumba yake alishambuliwa na
mume wake huyo kwa kumchoma na kitu
chenye ncha kari hadi kufa hapo na kisha
kutokomea kusiko julikana.

Wananchi walianza kutafuta mtuhumiwa
katika eneo hilo lakini  hakuweza kupatikana
licha wanakijiji hao kumsaka usiku kucha na
katika vijiji vya jirani
Kamanda Kidavashari alisema jeshi la polisi
linaendelea kumsaka mtuhumiwa ili atakapo
kamatwa afikishwe kwenye vyombo vya sheria
na ametowa wito kwa wananchi wa Mkoa wa
Katavi kuwa na utaratibu wa kuhakikisha kila
mkazi anakuwa na anwani inayo tambulika ili
anapo fanya uharifu aweze kupatikana kwa
urahisi.

Credits: Katavi Yetu