YAYA TOURE ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA

Yaya Toure akiwa na tuzo yake ya CAF aliyoshida jana jijini Lagos, Nigeria. Hiyo ni tuzo yake ya nne mfululizo.

Kiungo wa kati wa klabu ya Manchester city Yaya Toure ametangazwa kuwa mchezaji bora wa mwaka 2014 kutoka Afrika kwenye sherehe iliyofanyika huko jijini Lagos nchini Nigeria hapo jana.

Mchezaji huyo amechukua tuzohiyo kwa kuwashinda wachezaji Vicent Enyeama pamoja na Pierre Emerick Aubameyang.

Sherehe hizo zilihusisha na utoaji wa tuzo nyingine kwa washindi kama Mchezaji bora wa kike, Mchezaji bora mdogo wa mwaka,Timu bora ya taifa ya mwaka.

Hata hivyo mchezaji huyo ameweka rekodi ya kuchukua tuzo hiyo kwa vipindi mfululizo ambapo alichukua tuzo hiyo mwaka 2011,2012,2013,2014.


Tuzo zilizotolewa kwa ujumla

Mchezaji bora wa Afrika
Yaya Toure (Cote d'Ivoire and Manchester City)

Mchezaji bora wa Afrika wa ligi za ndani
Firmin Mubele Ndombe (DR Congo and AS Vita)

Mchezaji bora wa kike wa mwaka
Asisat Oshoala (Nigeria and River Angels)

Mchezaji bora mwenye umri mdogo wa mwaka
Asisat Oshoala (Nigeria and River Angels)

Mchezaji bora chipukizi
Yacine Brahimi (Algeria and Porto)

Kocha bora wa mwaka
Kheireddine Madoui (ES Setif)

Timu bora ya taifa ya mwaka:
Algeria

Timu bora ya wanawake ya mwaka
Nigeria

Klabu bora ya mwakaES Setif (Algeria)
Mwamuzi bora wa mwaka
Papa Bakary Gassama (Gambia)

Kiongozi bora wa mpira wa mwaka
Moise Katumbi Chapwe – President of TP Mazembe (DR Congo)

Tuzo kwa klabu kongwe

Oryx Club (Cameroon) – winners of the maiden edition of CAF Champions League 1964 Stade Malien (Mali) – runner up of the maiden edition of CAF Champion's League 1964


Tuzo za heshima

Dr Kwame Nkrumah (First President of Ghana)His Excellency Goodluck Jonthan (President of Nigeria)Kikosi bora cha Afrika cha mwaka

Mlinda mlango: Vincent Enyeama (Nigeria)

Mabeki: Jean Kasulula (DR Congo), Mehdi Benatia (Morocco), Stephane Mbia (Cameroon), Kwadwo Asamoah (Ghana)

Viungo: Yaya Toure (Cote d'Ivoire), Yacine Brahimi (Algeria), Fakhreddine Ben Youssef (Tunisia), Ahmed Musa (Nigeria)

Washambuliaji: Asamoah Gyan(Ghana), Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon)


Wachezaji wa akiba

Raïs M'Bolhi (Algeria), Firmin Mubele Ndombe (DR Congo), Ferdjani Sassi (Tunisia), Yao Kouasi Gervais 'Gervinho (Cote d'Ivoire), Abdelrahman Fetori (Libya), Akram Djahnit (Algeria), Roger Assalé (Cote d'Ivoire).