MAMA AUWA WATOTO WAKE WAWILI

(Tunaomba radhi kwa muonekano wa picha kuwa wa kutisha)


Katika hali isiyotegemewa watoto wawili wameuawa na mama yao , Zuhura Steven, anayedhaniwa kuwa anaupungufu wa akili na kufukiwa katika mashimo mawili tofauti, katika nyumba walimokuwa wakiishi, katika Mtaa wa Salimini Kata ya Chemchemu Manispaa ya Tabora.

Wakizungumzia tukio hilo linalodhaniwa kutokea kuanzia asubuhi ya Januari 25,2015, hadi majirani walipogundua tukio hilo usiku jana, Mwenyekiti wa Mtaa wa Barehani pamoja na wananchi walioshuhudia tukio hilo wanasema kuwamchana watoto hao hawakuonekana kama mazoea yao ambapo wamekuwa wakionekana kila siku nyakati za mchana wakicheza.

Jeshi la Polisi mkoani Tabora limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja marehemu kwa majina ya Mwamvua Mrisho (4) na Soud, (miezi 4) na upelelezi unaendelea pindi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.

Chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana na mtuhumiwa yuko mikononi mwa polisi hadi sasa.